Muslim Library

Surah Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter )

Swahili

Surah Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya count 60
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا ( 1 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 1
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا ( 2 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 2
Na zinazo beba mizigo,
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا ( 3 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 3
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا ( 4 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 4
Na zinazo gawanya kwa amri,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ ( 5 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 5
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ ( 6 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 6
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ ( 7 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 7
Naapa kwa mbingu zenye njia,
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ ( 8 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 8
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ ( 9 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 9
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ ( 10 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 10
Wazushi wameangamizwa.
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ ( 11 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 11
Ambao wameghafilika katika ujinga.
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ ( 12 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 12
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ ( 13 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 13
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ ( 14 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ( 15 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 15
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ ( 16 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ ( 17 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 17
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ ( 18 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 18
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ ( 19 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 19
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ ( 20 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 20
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ ( 21 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 21
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ ( 22 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 22
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ ( 23 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ ( 24 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ ( 25 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ ( 26 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ ( 27 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ ( 28 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ ( 29 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ ( 30 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ ( 31 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 31
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ ( 32 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 32
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ ( 33 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 33
Tuwatupie mawe ya udongo,
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ ( 34 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 34
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ( 35 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 35
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ ( 36 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 36
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ( 37 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 37
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ( 38 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 38
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ( 39 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 39
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ ( 40 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 40
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ ( 41 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 41
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ ( 42 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 42
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ ( 43 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 43
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ ( 44 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 44
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ ( 45 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 45
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ ( 46 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 46
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ ( 47 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 47
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ ( 48 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 48
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ( 49 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 49
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
فَفِرُّوا إِلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ( 50 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 50
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ( 51 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 51
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ ( 52 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 52
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ ( 53 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 53
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ ( 54 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 54
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ ( 55 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 55
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ( 56 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 56
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ ( 57 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 57
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
إِنَّ اللَّهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ ( 58 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 58
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ ( 59 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 59
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ ( 60 ) Adh-Dhariyat ( The Wind that Scatter ) - Aya 60
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah