Muslim Library

Surah Al-Fajr ( The Dawn )

Swahili

Surah Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya count 30
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَالْفَجْرِ ( 1 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 1
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍ ( 2 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 2
Na kwa masiku kumi,
وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ ( 3 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ ( 4 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 4
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ ( 5 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ( 6 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ ( 7 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ ( 8 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ ( 9 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ ( 10 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 10
Na Firauni mwenye vigingi?
الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ ( 11 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ ( 12 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 12
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ ( 13 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ( 14 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ ( 15 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ ( 16 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ ( 17 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ( 18 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا ( 19 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا ( 20 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا ( 21 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا ( 22 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ( 23 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ( 24 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ( 25 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ( 26 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ( 27 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 27
Ewe nafsi iliyo tua!
ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ( 28 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ( 29 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَادْخُلِي جَنَّتِي ( 30 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 30
Na ingia katika Pepo yangu.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah