Muslim Library

Surah At-Tur ( The Mount )

Swahili

Surah At-Tur ( The Mount ) - Aya count 49
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَالطُّورِ ( 1 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 1
Naapa kwa mlima wa T'ur,
وَكِتَابٍ مَّسْطُورٍ ( 2 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 2
Na Kitabu kilicho andikwa
فِي رَقٍّ مَّنشُورٍ ( 3 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 3
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
وَالْبَيْتِ الْمَعْمُورِ ( 4 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 4
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
وَالسَّقْفِ الْمَرْفُوعِ ( 5 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 5
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
وَالْبَحْرِ الْمَسْجُورِ ( 6 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 6
Na kwa bahari iliyo jazwa,
إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَاقِعٌ ( 7 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 7
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
مَّا لَهُ مِن دَافِعٍ ( 8 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 8
Hapana wa kuizuia.
يَوْمَ تَمُورُ السَّمَاءُ مَوْرًا ( 9 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 9
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
وَتَسِيرُ الْجِبَالُ سَيْرًا ( 10 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 10
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
فَوَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ( 11 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 11
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
الَّذِينَ هُمْ فِي خَوْضٍ يَلْعَبُونَ ( 12 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 12
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
يَوْمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا ( 13 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 13
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
هَٰذِهِ النَّارُ الَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ( 14 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 14
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
أَفَسِحْرٌ هَٰذَا أَمْ أَنتُمْ لَا تُبْصِرُونَ ( 15 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 15
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
اصْلَوْهَا فَاصْبِرُوا أَوْ لَا تَصْبِرُوا سَوَاءٌ عَلَيْكُمْ ۖ إِنَّمَا تُجْزَوْنَ مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ( 16 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَعِيمٍ ( 17 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 17
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
فَاكِهِينَ بِمَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ وَوَقَاهُمْ رَبُّهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ ( 18 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ( 19 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 19
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
مُتَّكِئِينَ عَلَىٰ سُرُرٍ مَّصْفُوفَةٍ ۖ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ ( 20 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
وَالَّذِينَ آمَنُوا وَاتَّبَعَتْهُمْ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَانٍ أَلْحَقْنَا بِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَمَا أَلَتْنَاهُم مِّنْ عَمَلِهِم مِّن شَيْءٍ ۚ كُلُّ امْرِئٍ بِمَا كَسَبَ رَهِينٌ ( 21 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
وَأَمْدَدْنَاهُم بِفَاكِهَةٍ وَلَحْمٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ ( 22 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 22
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
يَتَنَازَعُونَ فِيهَا كَأْسًا لَّا لَغْوٌ فِيهَا وَلَا تَأْثِيمٌ ( 23 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ غِلْمَانٌ لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ لُؤْلُؤٌ مَّكْنُونٌ ( 24 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ( 25 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 25
Wataelekeana wakiulizana.
قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ ( 26 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
فَمَنَّ اللَّهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ ( 27 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 27
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ( 28 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
فَذَكِّرْ فَمَا أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ ( 29 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ نَّتَرَبَّصُ بِهِ رَيْبَ الْمَنُونِ ( 30 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
قُلْ تَرَبَّصُوا فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ الْمُتَرَبِّصِينَ ( 31 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 31
Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
أَمْ تَأْمُرُهُمْ أَحْلَامُهُم بِهَٰذَا ۚ أَمْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ ( 32 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 32
Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
أَمْ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُ ۚ بَل لَّا يُؤْمِنُونَ ( 33 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 33
Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
فَلْيَأْتُوا بِحَدِيثٍ مِّثْلِهِ إِن كَانُوا صَادِقِينَ ( 34 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 34
Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ ( 35 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 35
Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ ( 36 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 36
Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَبِّكَ أَمْ هُمُ الْمُصَيْطِرُونَ ( 37 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 37
Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
أَمْ لَهُمْ سُلَّمٌ يَسْتَمِعُونَ فِيهِ ۖ فَلْيَأْتِ مُسْتَمِعُهُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ( 38 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 38
Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
أَمْ لَهُ الْبَنَاتُ وَلَكُمُ الْبَنُونَ ( 39 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 39
Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ ( 40 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 40
Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ ( 41 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 41
Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
أَمْ يُرِيدُونَ كَيْدًا ۖ فَالَّذِينَ كَفَرُوا هُمُ الْمَكِيدُونَ ( 42 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 42
Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
أَمْ لَهُمْ إِلَٰهٌ غَيْرُ اللَّهِ ۚ سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ( 43 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 43
Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
وَإِن يَرَوْا كِسْفًا مِّنَ السَّمَاءِ سَاقِطًا يَقُولُوا سَحَابٌ مَّرْكُومٌ ( 44 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 44
Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
فَذَرْهُمْ حَتَّىٰ يُلَاقُوا يَوْمَهُمُ الَّذِي فِيهِ يُصْعَقُونَ ( 45 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 45
Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
يَوْمَ لَا يُغْنِي عَنْهُمْ كَيْدُهُمْ شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ ( 46 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 46
Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا عَذَابًا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ( 47 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 47
Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
وَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعْيُنِنَا ۖ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ ( 48 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 48
Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
وَمِنَ اللَّيْلِ فَسَبِّحْهُ وَإِدْبَارَ النُّجُومِ ( 49 ) At-Tur ( The Mount ) - Aya 49
Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah